Thursday, July 31, 2008

Uraia wa nchi mbili
utaangamiza nchi,uzalendo..
-------
MNAOJALI kusoma historia na kazi za uandishi za watu wenye uchungu na nchi yao,
msikieni Shaaban Robert katika shairi lake,
“Fahari ya mtu”,akisema:
“Fahari ya kila mtu,kwanza ni taifa lake,Kutimiza wake utu,
afe au aokoe,Pasipo hofu ya kitu, halipendi liondoke

Fahari ya kila mtu,ya pili nchi yake,Mtu hakubali katu,
kutawaliwa pake,Hilo haliwi kantu,halina heshima kwake.

Fahari ya kila mtu,ya tatu ni nchi yake,Kuwaye chini ya watu,
wageni wa nchi yake,Ni jambo gumu kwa mtu,japo vipi aridhikie,
Pasipo nje. hofu ya kitu,hulipenda liondoke”.
Shaaban Robert.
Ni jambo la kuhuzunisha na kugadhabisha pia,kuona zama hizi,baadhi ya Watanzania wenzetu, hasa wanasiasa,wametekwa nyara na ubepari na mitaji ya kimataifa kiasi cha kupoteza uzalendo na moyo wa kuona fahari kwa taifa lao na kuabudu vya
Bofya na endelea>>>>>

No comments: