GARI LA RAIS

Hayo nimaneno ya mzee wa sumo.
Siri moja ya msingi sana katika maisha yetu ni kuhakikisha tunakuwa na mawazo kwamba inawezekana. Ukiamini, kwanza ni jambo la msingi, halafu mambo mengine yanafuatia. Ukiamini kwa uhakika kwamba nataka kuwa fulani, kisha ukaanza kuchukua hatua za kuelekea kule ambako unataka, kwa hakika hakuna jambo ambalo litakushinda.
Ninachotaka kieleweke hapa ni kwamba msingi wa maisha ya watu wengi ni nafsi zao, kama unakata tamaa, ndio kusema ni sawa na kifo, ni sawa na kusema aaah basi inatosha, kwa hiyo inakuwa ni mwisho wa kuendelea kuwaza tofauti juu ya kile ambacho umekuwa ukikiwaza.
Wakati fulani miaka minne iliyopita niliwahi kukutana na jamaa mmoja akawa anaomba ushauri juu ya namna gani anaweza kufanya ili kuhakikisha anaishi vizuri kwenye ndoa yake hasa baada ya kumfuma mkewe akiwa na wanaume wengine katika nyakati tofauti wakifanya ngono.
Watu wengi wanapokuwa kwenye uhusiano na wanapoona wenza wao labda wamekuwa na uhusiano na mtu au watu wengine, wanafikiria kutalakiana, lakini huko ni kukosea, unapaswa kukaa naye na kuzungumza naye, ili kujua msingi wa yeye kuwa vile, kisha angalieni mbele, namna gani mnaweza kwenda mbele katika hali ya mafanikio.
Kabla ya kuwa naye, kwa watu walio wengi ni kwamba waliwahi kuwa na watu au mtu mwingine, ni kweli inauma kusikia au kuona ana mwingine, lakini si sahihi kufikiria kutalikiana, cha msingi ni kukaa na kuangalia ni namna gani uhusiano wenu unaweza kuendelea kuwa mzuri, kwa kuondoa msingi wa mmoja kuwa hivyo, yaani kuanzisha uhusiano na mtu mwingine.
Katika uhusiano kuna mambo mengi ambayo unapaswa kuyazingatia, lakini leo tutayaangalia mambo 20, ambayo naamini kwamba kama kweli utayafanyia kazi kwa dhati, kwa hakika uhusiano wako utakuwa mzuri na wenye kuvutia, wala hutakuwa na majonzi tena, baadhi ya mambo hayo ni yafuatayo;
1. Ufanye ubongo wako kutafakari kwa makini yale malengo ambayo umekuwa ukiyawaza kabla ya kuoana kwenu. Je, umewahi kutaka ndoa ya namna gani na sasa unafanya nini?
Waza namna gani unaweza kuwa na ndoa nzuri. Kwa hakika ukifikiria hilo, utafanikiwa. Maisha yetu yanajengwa na fikra, ukiwaza mabaya, utapata mabaya, ukiwaza mazuri, kwa hakika utayapata.
2. Kama kwa mfano ndoa yako tayari imeingia shida, endelea kutafakari kwanini ina matatizo na nini nifanye iwe nzuri?
3. Zaidi, penda kufanya mazuri kwa mwingine, acha kuwaza aaah mbona mimi namfanyia mazuri, halafu yeye ananifanyia mabaya. Endelea kufanya mazuri mengi kwa mwenzi wako hata yeye anaonekana kufanya mabaya, hatimaye naye atakuwa mzuri, kwa maana ya kukufanyia mazuri pia.
Atawaza aaah huyu mtu mbona namfanyia mabaya tu, wakati yeye ananifanyia mazuri, mwishowe atabadilika, ndivyo inavyoaminika kitaalam.
4. Mfanye mwenzi wako ajione ni mwenye thamani na umuhimu mkubwa katika maisha yako. Je, unamthamini mwenzi wako? Tafakari, chukua hatua.
5. Mara zote tafakari ni nini ambacho nikimueleza mwenzi wangu atakuwa mwenye furaha?
6. Tafakari kabla ya kufanya au kuzungumza jambo. Wengi wa watu wanaharibu uhusiano kwa midomo na mikono yao, wakati mwingine unaweza kufikiri unamfanyia mtu kitu kizuri, kumbe sio.
Ni vizuri sana kulizingatia hili. Wakati mwingine kama huna la kuzungumza, ni vizuri kukaa kimya, kuliko kuzungumza 'utumbo'.
7. Shukuru kwa kile unachofanyiwa. Wakati mwingine yawezekana mwenzi wako anakufanyia kitu au anakununulia kitu, hata kama hukipendi, mshukuru kisha sema; �Lakini ukininunulia na kitu Fulani siku ukipata fedha nitapenda pia� Usionyeshe kudharau, hata kama labda amekununulia kitu ambacho kutoka moyoni hujapenda.
8. Uwe msikilizaji mzuri. Tena wakati mwingine kama mwenzi wako anazungumza jambo, tulia msikilize hata kama labda ulikuwa unachezea simu nk. Ni makosa makubwa kwa mfano mwenzi wako anazungumza halafu wewe uko bize na kitu kingine ambacho labda wakati huo si cha lazima kukifanya.
9. Jali hisia za mwenzi wako.
10. Acha kauli za kulaumu au kutusi waziwazi, kama mwenzi wako amekukosea, pata muda wa kukaa naye faragha. Ni makosa makubwa kumtusi au kumsema mtu waziwazi, hapo ndipo huzaliwa mabaya mengi, baadhi yake ni vile unaweza kuona watu wakati fulani wakipigana waziwazi�kitaalam watu huwa hawako tayari kudharauliwa hadharani.
11. Acha kuwaza mambo yasiyowezekana. Kwa mfano ni makosa kuamini kuwa katika ulimwengu huu unaweza kumpata mwanamke au mwanaume ambaye ni msafi au mzuri asiye na makosa kwa asilimia mia. Kama unafikiria hilo, ni vizuri ukakaa pasipo kuoa au kuolewa, kwa sababu hayuko, hata Mungu anajua hilo.
Wakati mwingine baadhi ya mambo si makosa, bali yako tofauti na vile ambavyo tungependa iwe, kwa mfano wako watu wangependa kuona dunia haijaumbwa kama hivi ilivyo leo nk, japo ndio uamuzi wa Mungu.
12. Usitoe menno yenye kusababisha maumivu. Kama inatokea mwenzi wako anazungumza maneno yenye kusababisha maumivu, zungumza maneno mbadala, usikuze maumivu. Ongeeni kama watu mliokomaa, acheni kuendekeza migogoro.
13. Zifahamu vema tabia za mwenzi wako na namna gani unaweza kufanya ili kuhakikisha uhusiano wenu unakwenda mbele.
14. Badala ya kuwa na kitabu cha makosa ambayo mwenzi wako anayafanya, ni vizuri ukawa na daftari la mambo mazuri, ambayo mwenzi wako anakufanyia. Tafakari mazuri, zaidi kuliko makosa.
15. Andika tabia nzuri za mkeo au mumeo, badala ya labda sura yake mbaya nk.
16. Angalia ni namna gani unaweza kumfanya mwenzi wako kuwa na tabia nzuri zaidi ya alivyo sasa.
17. Uwe tiba kwa matatizo ya ndoa na uhusiano wenu kwa ujumla. Acha tabia ya kulalamika, kuipiga kelele ovyo.
18. Kumbukeni nyakati zile za furaha na fikra ambazo mmekuwa nazo kuhusu uhusiano wenu. Ongezeni manjonjo yale ya kupendana, na si kufikiria mabaya tu kama ilivyo kwa baadhi ya watu.
19. Angalieni ni namna gani mnaweza kushirikiana katika kuimarisha uhusiano wenu, pia angalieni namna ya kushirikiana katika kazi mbalimbali hasa biashara nk.
20. Ishi kana kwamba unakufa kesho. Mabaya yaliyofanyika jana acha yabaki kuwa ya jana, wala msiyape nafasi kuendelea kuwaumiza vichwa na akili zenu.
Waza leo na kuendelea mbele, achana na jana. Kumbuka watu walikuwa wanatambaa, leo ni watu wazima wanatembea, maisha ni mabadiliko, mtu anaweza kuwa mbaya leo, kesho akawa mzuri, na kinyume chake
CONTACT PERSON: Mr. Mustafa Hassanali
TELEPHONE NUMBER: +255-78-4303880
EMAIL ADDRESS: media@swahilifashionweek.com
WEBSITE URL: http://www.swahilifashionweek.com
Inaugural “Origin Africa Designer Showcase”
Two Designers present Tanzania
Collection Made from Local Fabrics Made in Tanzania
Inaugural “Origin Africa Designer Showcase” had be held on 28 April 2010 in Nairobi at the Laico Regency. It is hoped that this will promote opportunities for local talent and local manufacturers to work together to develop a strong African fashion industry.