Wednesday, October 27, 2010

mpoto asherehekea siku yake ya kuzaliwa na watoto yatima

Mrisho Mpoto akikabidhi msaada wa vyakula kwa mlezi wa watoto yatima.

Mwanamuziki wa miondoko ya kizazi kipya MRISHO MPOTO amewataka wadau mbalimbali kuwasaidia watoto yatima kielimu na kiuchumi hatua itakayosaidia watoto hao kufikia malengo yao kimaisha

Mrisho Mpoto amesema hayo wakati akisherekea siku yake ya kuzaliwa na watoto wa kituo cha CHAWAMA kilichopo SINZA jijini DSM ambapo pia amekiri mchango wa watoto wadogo katika mafanikio yake kimuzik.

Naye mlezi wa kituo hicho SAIDA HASSAN ameshukuru watu mbalimbali wanaovutwa kujua mahitaji ya watoto yatima na kutoa misaada yao hali iliyomfanya ashindwe kujizuia na kuwaombea Dua kwa mola.Zaidi Bofya Hapa

Baada ya hapo basi na tuburudike na wimbo wake wa Adella unaofanya vyema kwa sasa katika anga ya muziki hapa bongo


No comments: