Monday, October 4, 2010

Ajali mbaya sana yatokea kinondoni jioni ya jumamosi.
Gari aina ya Subaru lenye namba za usajiri T 193 AZL ikiwa katika hali mbaya sana mara baada ya kupata ajali jioni ya jumamosi maeneo ya Kinondoni,Ubalozi wa Ufaransa.gari hii ambayo ilikuwa ikitokea maeneo ya Kinondoni Morocco kuelekea mjini,ilipoteza muelekeo mara baada ya gari moja kuingia ghafla katika barabara kubwa huku gari hii ikiwa katika mwendo wa kasi sana na kumfanya dereva wa gari hii kushindwa kuikontroo gari hii na kwenda kugonga moja ya nguzo za taa za barabarani na kuifanya ikapinduka.ndani ya gari hii kulikuwemo na watu watatu ambao wawili walijeruhiwa na kukimbizwa hospital na mwingine kufanikiwa kutoka bila jeraha lolote.
Sehemu iliyokuwepo nguzo ya taa za barabarani iliyogongwa na gari hiyo na kuifanya ikang'oka kabisa katika sehemu yake.
Mmoja wa waliokuwemo ndani ya gari hiyo (anaetumia simu) ambaye hakutaka kutaja jina lake akijaribu kuwasiliana na ndugu na jamaa kuhusiana na ajali hiyo iliyowakuta.
Askari wa Usalama barabarani,akipata maenezo mafupi toka kwa mashuhuda wa ajali hiyo.

No comments: