Wednesday, October 7, 2009

miriam gerald ndiye vodacom miss TZ 2009 na pia ndiye Redds miss photogenic!!!
Miriam akiwa ameongozana na mabodigadi wataomlinda wakati wa hafla akipunga mikono wakati wa fainali hizo ukumbi wa Mlimani City Conference Hall jijini Dar baada ya kutangazwa Redds Miss Photogenic 2009, shindano ambalo liliratibiwa na Globu ya Jamii na kudhaminiwa na Redds Original. Zawadi yake ni sh. milioni moja, kutengenezewa jarida (portfolio) ya weledi ya urembo pamoja na mkataba wa mwaka mmoja wa kufanya kazi za umodo na kampuni inayoongoza ya uwakala wa umodo ya Beautiful Tanzanie Agency
Miriam akiwa katika kiti chake cha enzi baada ya kutawazwa Vodacom Miss TZ 2009
Nasreem Kareem akijiandaa kumvisha taji Miriam ambaye wanatoka naye jiji la Mwanza
Nasreem Kareem akimvija taji Miriam
Nasreem akimvisha sasha la pili Miriam la Miss TZ 2009 juu ya lile la Redds Miss Photogenic 2009
Balozi Ami Mpungwe akionesha taji la Vodacom Miss TZ ambalo limetengenezwa kwa Tanzanite

Miriam na warembo wenzie waliofikia tano bora
miriam gerald ndiye Vodacom miss TZ 2009 na pia ndiye miss Redds Photogenic 2009 kwa mujibu wa matokeo ya fainali hizo zilizohitimishwa katika ukumbi wa Mlimani City Conference centre jiijini Dar .

Kwa habari kamili pamoja
na picha na video kibao...
BOFYA HAPA

pamoja na yote hayo ila sikufurahishwa na jambo dogo sana ambalo waandaaji hawakuliangalia. Nalo niyale mafataki waliyo yalipua hawakutoa tahadhari maana milio ilikuwa mikubwa ndugu zangu kule Mabibo walizisikia . Maana kuna watu walipatwa na kihoro katika milio hiyo .
Maoni yangu linapofanyika swala kama hili watu wanaoishi jirani waambiwe pia wasije wakakimbia makazi yao bure na kusababisha hayo yalio tokea katika kilele cha usiku wa kumtafuta mrembo wetu.
Kwa mengine yote nawapa hongera wote mlioshiriki na mkulipa unadhifu.
Na mwisho mwanza mwanza wako juu hongereni sana. wazee wa mapanki!!

No comments: