Wednesday, April 21, 2010

Kama umjuavyo Kocha wa Inter Milan Jose Mourinho( special one ) kulia akishangilia na mchezaji wake pamoja na maafisa wa timu hiyo usiku wa kuamkia leo baada ya kuifunga Barcelona magoli 3-1.

Inter wameweza kujiweka vizuri katika mashindano ya ubingwa wa ulaya
kwa kuwafunga mabingwa watetezi Fc Barcalona kwa magoli 3-1 katika uwanja
wa stadio meazza de san siro milano usiku huu na kujiweka kaatika matumaini
ya kucheza fainali itakayofanyika Madrid Spain.

Mchezo ulikuwa wa kiufundi
haswa kutokana na uchezaji mzuri wa timu ya Barça lakini kwa usiku huu walishindwa
kabisa kuukabili mchezo wa nguvu wa timu ya Fc Inter ambao waliweza kuwabana
vuzuri uwanjani. Barçalona ndio waliokuwa wa kwanza kuandika bao lililofungwa na
mchezaji chipukizi Pedro rodriguez katika dakika ya 19 kipindi cha kwanza.


Dakika ya 30 kipindi cha kwanza snejder aliweza kuisawazishia timu yake ya Inter,na
kipindi cha pili dakika ya 48 maicon aliongeza bao la pili na Diego milito mnamo dakika ya
61 aliweza kuandika goli la tatu ambalo wachezaji wa barçalona walipinga vikali wakidai
limefungwa kwa kuotea.mechi ya marudiano itafanyika mjini Barçalona tarehe 28/4 ya
mwezi huu
sasa kazi ipo mechi ya marudiano maana Barcelona walionyesha kiwango ball position wao walikuwa na alama za juu kama ingekuwa kuangalia hiyo jna barcelona wangeshinda lakini raha ya mechi bao Inter waliweza kufanya hilo .
Hongera watot o wa special one.

No comments: