Friday, November 20, 2009

mpoki apata ajali
Mpoki, mwigizaji maarufu wa kundi la Ze Original Komedy (kulia) amepata ajali ya gari usiku wa kuamkia jana, na inasemekana amevunjika mkono wake wa kushoto ambapo mfupa umeachia.
Habari kutoka ndani ya kundi hilo zinasema hali yake sio mbaya sana na jana aliruhusiwa kwenda nyumbani kutoka hospitali ya Kairuki iliyoko mikocheni jijini Dar, na ataendelea na matibabu akiwa nyumbani.
Ajali hiyo ilitokea mikocheni wakati gari alilokuwa anaendesha lilipogongana uso kwa uso na Rav4 iliyokuwa inaendeshwa na mwanamama ambaye naye kalazwa hospitali ya TMJ.

No comments: