Thursday, October 21, 2010

onyesho la mavazi la swahili fashion week kuanza novemba 4,2010
Mbunifu wa Mavazi na Muandaaji wa onyesho la mavazi la Swahili Fashion Week,Mustafa Hassanali akizungumza mbele ya wandishi wa habari leo asubuhi ndani ya hoteli ya Southern Sun kuhusiana na uzinduzi wa onyesho hilo litakaloanza kurindima novemba 4 mpaka 6 ndani ya viwanja vya Karimjee hall.Kutoka kulia ni Mratibu wa mitindo Bw.Washington,Muwakilishi wa hoteli ya Southern Sun Bi.Judith Muyo,na kushoto kabisa ni Alex Galinoma kutoka EATV pamoja na Afisa habari wa tamasha la Swahili Fashion week,Bi Saphia Ngalapi.


Kwa mara ya tatu sasa Swahili Fashion Week itafanyika Karimjee Hall kuanzi tarehe 4 hadi 6 November 2010, Dar Es Salaam , Tanzania .

Swahili Fashion Week itawaleta pamoja wabunifu wa mavazi 24 kutoka nchi zinazoongea lugha ya Kiswahili ili kuweza kuonyesha ubunifu wao katika kubuni mavazi ya aina mbalimbali kwa kutumia aina mbalimbali za malighafi.

Wabunifu watakaoonesha mavazi katika Swahili Fashion Week kwa mwaka huu ni pamoja na Ailinda Sawe, Manju Msita, Kemi Kalikawe, Christine Mhando, Shellina Ibrahim, Farha Naaz Sultan, Gabriel Mollel, Robi Morro, Asia Idarous, Zamda George, Khadija Mwanamboka, Jamilla Vera Swai and Made by Afrika. wabunifu kutoka Kenya ni Sonu Sharma, Moo Cow, KiKoromeo, John Kavike na Kooroo, na kutoka Uganda ni mbunifu Stella Atal.

“Pamoja na maonyesho ya mavazi, mwaka huu Swahili Fashion Week itakwenda sambamba na tamasha la maonyesho ya bidhaa mbalimbali zenye asili ya mswahili kutoka mwambao wa Afrika mashariki”. Alisema Mustafa Hassanali muaandaaji y tukio la Swahili Fashion Week.

“Tunafungua milango zaidi kwa ajili ya watazamaji wapya wa Swahili Fashion Week, amboa watapata fursa ya kununua bidhaa mbalimbali. Tamasha hili ambalo linazileta pamoja bidhaa mbalimbali za sanaa na utamaduni wa mswahili, pia litahamasisha ubunifu zaidi katika bidhaa zinazokwenda sambamba na maisha halisi ya jamii ya watu wanaoongea lugha ya Kiswahili kwa kukutana pamoja na kubadilisha mawazo na kujifunza uzoefu mpya katika masuala yanayohusiana na sanaa kwa ujumla.” Aliaongeza Hassanali.

Pamoja na maonyesho, pia kutakuwepo aina tofauti za burudani kutoka kwa vikundi

Mbalimbali vya muziki, uchoraji wa hina, usukaji mikeka, sambamba na semina za aina tofauti zitakazo washirikisha wabunifu wa mavazi.

Aidha Swahili fashion Week imeandaa aina tofauti za zawadi zitakazotolewa mwaka huu kwa lengo la kutambua na kuthamini vipaji vya aina mbalimbali vitakavyooneshwa, ikiwa ni pamoja na zawadi ya mwaka kwa mbunifu anaechipukia.

Swahili fashion week 2010 imedhaminiwa na Home of Swahili Fashion week Southern Sun, Origin Africa, USAID Compete, EATV, East Africa Radio, Malaria Haikubaliki, BASATA (Baraza La Sanaa Tanzania) Ultimate Security, Monier 2000, Colour Print ltd, Global Outdoor Ltd, Amarula, Vayle Springs Ltd, ZG Films, Darling Hair, Danish make up designs, Nipashe, Bilicanas, Perfect Machinery LTD, 1 & 1 internet solutions, Sengi Tours, Ifashion na 361 Degrees.

Tuesday, October 19, 2010

Dr alivyoipasua nzega na kahama kwenye kampeni zake za urais

Dk. Willibrod Slaa akihutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Kahama mjini Kahama, mkoani Shinyanga jana jioni.
Dk. Willibrod Slaa akisalimiana na baadhi ya watawa waliohudhuria mkutano wa kampeni zake kwenya Uwanja wa Sabasaba mjini Nzega jana asubuhi.
Dk. Willibrod Slaa akihutubia katika mkutano wake wa kampeni kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Nzega, Tabora.

mr II nae aendelea kupasua miamba ya kampeni.

Mgombea ubunge wa jimbo la Mbeye Mjini kupitia tiketi ya chama cha CHADEMA,Joseph Mbilinyi a.k.a Mr II a.k.a Sugu akiwahutumia maelfu ya wakazi wa Mwanjelwa,Mkoani Mbeya hivi karibuni,hiyo ikiwa ni sehemu yake ya lala salama za kampeni ambazo zinaelekea ukingoni kwa hivi sasa.

kampuni ya TCC YAFADHILI MAFUNZO YA MAOFISA WAANDAMIZI WA POLISI MAREKANI

Mkurugenzi wa Oparesheni wa Jeshi la Polisi, Kamishna Paul Chagonja (wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na maofisa watatu wa Jeshi la Polisi waliokabidhiwa tiketi na fedha za kujikimu ili kuweza kuhudhuria Mkutano wa Kimataifa wa Maofisa wa Polisi utakao fanyika Oktoba 22-28 mwaka huu katika mji wa Oralndo , Florida nchini Marekani.Wengine kutoka kushoto ni SACP.Jamal Rwambow, ACP, Renatus Mbushi,ASP.Emmanuel Mkilia na Mkurugenzi wa Mahusiano wa Kampuni ya Sigara Tanzania, Paul Makanza aliyekabidhi udhamini huo. TCC imekuwa ikiwadhamini maafisa mbalimbali wa Jeshi la Polisi kuhudhuria mkutano huu tangu mwaka 2001.( Picha na Executive Solutions.)

meli ya hospitali ya china yatia nanga dar,kutoa matibabu bure kesho.


MKUU wa Hospitali Kuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Lugalo, Meja Jenerali Salim Salim, akipewa zawadi maalu na Kamanda wa Meli ya China, yenye vifaa na madaktari wa kutoa huduma za matibabu,Bao Yuping, alipotembelea meli hiyo leo katika Bandari ya Dar es Salaam.
MGANGA Mkuu wa Hospitali Kuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ya Lugalo, Meja Jenerali Salim Salim, akionyeshwa machine ya upimaji magonjwa ya moyo iliyomo katika meli ya China, alipotembelea meli hiyo leo, katika Bandari ya Dar es Salaam, ambako imetia nanga ikiwa na madaktari watakaotoa huduma ya matibabu kwa wagonjwa mbalimbali hapo kesho. Kushoto ni Kamanda wa meli hiyo, Bao Yuping na kulia ni Balozi wa China hapa nchini Liu Xinsheng.Kwa habari na picha zaidi kung'uta hapa.

Saturday, October 9, 2010

hoja ya haja toka kwa US Blogger
Gharama ya kura yangu

Ndugu Watanzania. Mwaka huu wa-Tanzania tumepata tena nafasi ya kufanya maamuzi magumu nchini mwetu, maamuzi ya kuchagua viongozi watakaokuwa na majukumu ya kutuendeleza kama Taifa.

Ninaamini swala la uchaguzi ni zito na muhimu sana na kila mmoja wetu ana wajibu mkubwa wa kuwa makini kwa sababu uzembe katika kupiga kura huzaa uongozi wa kibabaishaji na ni ndoto za alinacha kutegemea viongozi wabovu, wapenda rushwa na wasio na sifa kuleta mabadiliko yoyote.

Natambua kila mmoja wetu ana vigezo vyake vya nani atakayempa kura zake, nimeona niwaeleze vigezo vyangu ili tuweze kubadilishana mawazo.

Urais:
Anayekubali midahalo; Ninaamini Rais anayenifaa ni yule amabaye anaelewa matatizo ya kitaifa na mwenye upeo wa kuelewa nini kifanyike katika kukabiliana na matatizo hayo. Ili niweze kumtathmini na kumpima na wagombea wengine lazima awe tayari kuingia kwenye midahalo ili nikiwa kama mpiga kura nipate nafasi ya kumhoji. Siko tayari kumpigia kura mgombea anayefanya kampeni kama tape recorder, yaani anakuja jukwaani kusema anayotaka yeye tu na kuondoka.

Elimu ya Bure; hakuna taifa linaloweza kuwa na mategemeo ya maendeleo bila ya kuwaelimisha wananchi wake. Tanzania ya leo inakabiliwa na tatizo la masikini kuendelea kuwa masikini na matajiri wanazifi kuwa matajiri, njia muhimu ya kuwakomboa walio wengi ni kuwapa elimu yenye manufaa wananchi wote. Siko tayari kukubali hoja ya kwamba haiwezekani, nataka kiongozi ambaye anathubutu kubana matumizi yasiyo ya lazima ya Serikali kama magari ya fahari ili elimu ipatikane.

Uwajibikaji kifedha; Nataka Rais ambaye hawachekei wahalifu wenye tabia ya kudokoadokoa fedha za umma. Fedha za umma zitumike kwa kile kilichokusudiwa tu na kwa kufuata taratibu zilizopo . Nimechoka kusikia ripoti za kitaalamu zinazothibitisha wizi na Rais hawaagizi wasaidizi wake kuwapeleka wahusika kwenye vyombo vya sheria. Matatizo yetu mengi yangeweza kupungua endapo matumizi ya fedha za umma yangeboreshwa.

Serikali iliyo wazi; nimechoshwa na tabia ya kuendesha kazi za Kiserikali kisiri kama kibaka anayekwenda kuiba usiku wa manane. Nakataka Rais atakayetuletea Sheria inayogusa maswala ya Open Records ambayo inamruhusu kila Mtanzania kupata taarifa zinazohusu maamuzi ya Serikali. Kama Serikali imetoa zabuni kwa kampuni yoyote basi tuwe na nafasi ya kujua undani kama vile makampuni mangapi yaliomba tenda, vigezo gani vilitumika, etc. Kwa mikataba ambayo inaweza kuwa ya siri kama ya kiusalama nayo iwe monitored na kamati ya uchumi ya Bunge ili angalau tuwe na wabunge watakaotuwasilisha kudhitibi utoaji wa zabuni.

Uchumi na Biashara; Kabla ya uhuru tulikuwa ni wazalishaji wa malighafi kwa ajili ya mataifa makubwa, leo hii baada ya karibu miaka 50 bado tunafanya hayohayo. Nataka rais mwenye jibu ya kubadilisha Tanzania kutoka nchi inayozalisha malighafi na kuwa taifa linalozalisha bidhaa za viwango vya juu zilizokamilika.

Serikali na Bunge; Kuna haja ya kuwa na mapinduzi ya katiba. Katiba ina matatizo kadhaa, moja wapo ni hili ya wabunge kuwa mwaziri. Kwa mtizamo wangu hii ni conflict of interest kwa sababu haiwezekani wabunge wajidhibitu wenyewe, tunahitaji clear separation ya hizi nguzo mbili za dola. Mfumo wa sasa hauthamini fedha za walipa kodi, mfano sasa hivi mawaziri wako majimboni kwenye kampeni lakini Serikali inawalipa mamilioni ya mishahara. Wakirudi maofisini Serikalini hawaonekani majimboni mpaka wakati wa uchaguzi ujao wakati wanalipwa fedha kama wabunge. Hawa wanatafuna fedha za bure kwa kuwa haiwezekani wafanye kazi mbili zinazohitaji muda mwingi. Mfumo huu unatumaliza.

Kuimarisha mahakama; leo hii mahakama zetu zinakabiliwa na matatizo ya kdaji kutokana na ukata. Nataka Rais ambaye atahakikisha mahakama zetu zinapata bajeti ya kutosha ili wananchi wapate haki zao katika kipindi muafaka.

Katika nafasi ya Ubunge halikadhalika kura yangu itakwenda kwa Mbunge anayeunga mkono matakwa haya.

Je, wewe una masharti gani kwa anayetaka kura yako?

By US Blogger
Usblogger11@gmail.com
service road barabara ya mandela road
Ankal pole kazi
Naomba kuuliza. Hivi hii sehemu ya barabara service road inamaanisha ku-service vimeo ama vipi. Mfano huyu jamaa ndo kageuza garage hapo. Naomba kugahamishwa
Sent from my BlackBerry® smartphone from Vodacom

Monday, October 4, 2010

Ajali mbaya sana yatokea kinondoni jioni ya jumamosi.
Gari aina ya Subaru lenye namba za usajiri T 193 AZL ikiwa katika hali mbaya sana mara baada ya kupata ajali jioni ya jumamosi maeneo ya Kinondoni,Ubalozi wa Ufaransa.gari hii ambayo ilikuwa ikitokea maeneo ya Kinondoni Morocco kuelekea mjini,ilipoteza muelekeo mara baada ya gari moja kuingia ghafla katika barabara kubwa huku gari hii ikiwa katika mwendo wa kasi sana na kumfanya dereva wa gari hii kushindwa kuikontroo gari hii na kwenda kugonga moja ya nguzo za taa za barabarani na kuifanya ikapinduka.ndani ya gari hii kulikuwemo na watu watatu ambao wawili walijeruhiwa na kukimbizwa hospital na mwingine kufanikiwa kutoka bila jeraha lolote.
Sehemu iliyokuwepo nguzo ya taa za barabarani iliyogongwa na gari hiyo na kuifanya ikang'oka kabisa katika sehemu yake.
Mmoja wa waliokuwemo ndani ya gari hiyo (anaetumia simu) ambaye hakutaka kutaja jina lake akijaribu kuwasiliana na ndugu na jamaa kuhusiana na ajali hiyo iliyowakuta.
Askari wa Usalama barabarani,akipata maenezo mafupi toka kwa mashuhuda wa ajali hiyo.

Sunday, September 26, 2010

Amazing Facts About Honey

Below are 10 amazing facts about honey that most people have no idea about. It is amazing what kind of health benefits can be found in foods given to us by mother nature herself. Simply adding natural foods like honey in place of more fattening options can make your body feel fresh and rejuvenated. Take a moment to read through all of these interesting facts about honey and see if you learn something interesting.
1. Honey is the only non man-made sweetener which also is considered to have healing effects.
2. Honey has a pH level around 3-4 and consists of roughly 18% water. Because of this honey is a very stable substance and can last hundreds of years if properly stored.
3. Honey can reduce fat deposits found in our cardiovascular system.
4. Honey will not ferment in your stomach like refined table sugar or sucrose does. Because of this it does not subject you to a risk of bacterial infection.
5. Honey is the simplest possible molecular form of sugar, which cannot be broken down any further. This allows it to travel directly from the small intestine to the blood stream while not causing any problems to the digestive system like sucrose.
6. Honey is a top choice as fuel for burning body fat during sleep since it has an equal ratio of fructose to glucose.
7. Honey is the best substance to use to treat burns. Honey can effectively subdue pain while quickly healing a wound without scarring.
8. Vitamins as well as antioxidants are found in honey. One special antioxidant known as ‘pinocembrin’ is found only in honey.
9. Honey is known to be a very effective and safe solution to children’s coughs, even more so than over-the-counter medicines.
10. Some recent studies have shown that athletes who consumed honey before and after physical activity have recovered faster than those athletes who did not consume any honey at all.
Given your new found knowledge of honey, now hopefully you can use it’s health benefits to your advantage. Keep in mind, the more natural the honey, the better. The honey found at your local fast-food chain is not going to give you the same health benefits as fresh natural honey straight from the bees nest. Start adding small amounts of natural honey to your meals to enjoy the health benefits it can offer you.