Wednesday, February 24, 2010

China hawataki kuona hii picha kwa nini??




Portugal is expected to announce three days of national mourning following the floods that have hit Madeira island, killing 42 people.

Officials say the announcement will be made at an emergency cabinet meeting convened to discuss the crisis.

Search teams are continuing to look for victims amid debris, after mud and rock swept through towns on Saturday.

Cars were buried, buildings damaged, and people swept along in raging waters through the regional capital, Funchal.for more details click here.

Terry staying focused on football

Terry: Put personal problems behind him
John Terry says his "broad shoulders" have allowed him to forget his personal problems and focus on winning honours with Chelsea and England.

Tuesday, February 23, 2010

Kipanyaa na Busara zake ..
mhh hapa kunani naomba kichwa cha picha ?
Dawa ya Kulevya Yaliyohifadhiwa kwenye
Vinyago yakamatwa

Ma


Kamanda wa Polisi wa viwanja wa vya ndege nchini,Kamishna msaidizi Mwajuma Kiponza(kulia) akiwaonyesha waandishi wa habari jana madawa yakulevya yaliyokuwa yameifadhiwa kwenye vinyago.Madawa hayo yalikamatwa kutoka kwa mtuhumiwa anayejulikana kwa jina Halid Maunga juzi katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere alipokuwa akijiandaa kuyasafirisha kwenda Uingereza.
du wadau wa blog hii imekaaje ndio zinavyopitishwa watu wakamchoma leo au jamani nisaidie mawazo katika hili .
bongo darisalaaaaam...
Bwana Kadidi2i,
Kuna jambo ambalo limenitokea nikaamua kulileta kwako ili uweze kulitoa kwenye blog yetu ya hii huenda itasaidia wadau wengine manake hata mimi huaga najifunza mambo mengi sana kutoka kwenye blog hii.

Siku ya jmosi nilienda mjini kidogo kufanya shopping ya bidhaa nilizunguka sana nikapata kiu ya maji bahati nzuri nilipokua napita mitaa ya kisutu nikakutana na muuza maji alikuwa amebeba kwenye box lake maji ya aina ya uhai ikabidi ninunue alikua amebeba yale ya shilling 300/=.Nikanywa harakaharaka kwa sababu nilikua na kiu kali.

Baada ya kumaliza sikukitupa hicho kichupa cha plastic maaana sikuona mahali pa kutupia kwa hiyo nikaamua niende nacho mpaka nipate mahali pa kutupia.Nikawa nimekishika mkononi mara wakati naichezea mkononi nikahisi mikwaruzo kuangalia kumbe kile kichupa kilikuwa kimetumika nilipoangalia kwa makini ndani ya chupa nikaona uchafu na juu ya mdomo wake nikaona uchafu mweupemweupe...
Nakuambia,Michuzi niliishiwa nguvu.Nikapata mstuko mkubwa nikaenda mpaka pale mtaa wa Samora nilipokua nimepaki gari nikawa nimeduwaa sijui lakufanya.Wale vijana wanaokaaga pale kuongoza magari kupaki na saa nyingine kuosha magari wakaniuliza vipi?Nikawaeleza mkasa wote wakacheka sana wakaniambia umekunywa maji ya bomba sasa kilichobaki nikuomba Mungu usipate typhod.
Sasa wakaanza kunielimisha. Wakanieleza namna hayo maji vijana wa mjini wanavyoyatengeneza.
Kuna njia kuu mbili. Moja ni kuwa wanaokota hayo sijui niite makopo au vichupa vya plastic sehemu mbalimbali jijini wanajaza maji ya bomba au maji yoyote watakayopata halafu wanaenda kiwandani wananunua mifuniko pamoja na seal zake kabisa wanakuja wanasokomeza hiyo mifuniko pamoja na seal kwenye hivyo vichupa sasa wewe ukija kununua hayo maji ukafungua huo ufuniko lazima ikate seal kwa hiyo unapata imani unakunywa.

Njia ya pili wanaokota hivyo vichupa pamoja na mifuniko wanafungua wanajaza maji halafu wanachukua super glue wanaizungushia katikati ya mfuniko na seal yake wewe ukija kununua ukafungua utaona unakata seal kumbe ni super glue unakata.

Hii kitu ni hatari sana manake vichupa vyenyewe wameokota na hata kuviosha havijaoshwa kwa hiyo hapo mtu unakua na risk ya kupata TB,Typhod na magonjwa ya matumbo Kipindupindu.

Kwa hiyo wadau kuweni waangalifu na maji ya barabarani hasa ,wale vijana wanaobeba maji mikononi ambao wako katika mitaa mingi ya jijini Dar-es Salaam.Mfano maeneo hayo ya kisutu,kwenye mataa ya pale faya,manzese,ubungo na sehemu nyingine nyingi hasa zile sehemu zenye vituo au kwenye mataa.

Wako katika mitaa mingi ya jijini Dar-es Salaam.Mfano maeneo hayo ya kisutu,kwenye mataa ya pale faya,manzese,ubungo na sehemu nyingine nyingi hasa zile sehemu zenye vituo au kwenye mataa.
tutazzzzzz
Habari za leo Mdau,
NAOMBA NIWEKEE KWA WADAU
Nimatarajio yangu wote ni wazima na mnaendelea vizuri na kazi. Kwa kipindi cha miezi kadhaa sasa nimejaribu kufuatilia adha kubwa tunayoipata sisi Wakazi wa Temboni, Kwa Msuguri, Mbezi, Kibamba na kuendelea along Morogoro Road.
Kero hii kubwa hasa nyakati za asubuhi (saa 11 alfajiri na saa 2 asubuhi) na jioni (kuanzia saa 10 hadi saa 3 usiku) huwa inasababishwa na TUTA (BUMP) lililowekwa na TANRORADS eneo la Kimara Stop-Over.
Yes, I agree with Kinondoni Municipal Council na wadau wengine idea ya kuwa na hili tuta ni kupunguza mwendo kasi wa Mabasi, Malori, Daladala,Taxi Drivers n.k. Lakini ukifuatilia kwa karibu zaidi utaona hakuna tija yoyote inayopatikana na uwepo wa hili tuta pasi na kusabibisha unnecessary traffic congestion.
Wadau hii kero inaongezeka day by day na ni hakika siku moja it will reach its climax na kusababisha usumbufu mkubwa kwa Wananchi. Nafikiri ni vyema sasa Wadau tukajipanga na kwenda kumwona Manager wa TANROADS - DSM na kukaa naye meza moja ilikuweza kutatua kero hii kubwa.
I know kila mtu anayetumia barabara hii anaguswa na kero hii na huwa tunazungumza zungumza tu mitaani bila ya kufuatilia kwenye ngazi husika. Nafikiri ni sasa ni muda muafaka tukahamasishana na kwenda TANROADS ili kuweza kupata ufumbuzi. Ndugu mdau, the above is my opinion naomba opinion yako ili tuweze kujua way forward.
Regards, Mdau Albert

Monday, February 22, 2010

tiger woods

JK: Uhusiano wetu na China ni kwa maslahi yetu wenyewe
Na Mwandishi Maalumu, Turkey
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa msukumo wa sasa wa kuwapo kwa uhusiano wa karibu zaidi kati ya nchi za Afrika na China unatokana na mahitaji halisi na maslahi ya kweli kweli ya Bara la Afrika na wala siyo na itikadi.

“Bara la Afrika linatafuta masoko kwa bidhaa zake. Bara la Afrika linatafuta mitaji na uwekezeji katika chumi zake. Bara la Afrika linatafuta teknolojia kwa ajili ya maendeleo yake. China iko tayari kutoa hayo yote. Sasa nongwa iko wapi?” Rais Kikwete amewauliza waandishi wa habari wa Uturuki.

Rais Kikwete alikuwa anazungumza , Jumamosi, Februari 20, 2010, na waandishi wa habari wa vyombo vya habari vya Uturuki baada ya kuwa amefungua Mkutano wa Pili wa Wafanyabiashara wa Tanzania na Uturuki kwenye Hoteli ya Grand Cehavir mjini Istanbul.

Kiasi cha wafanyabiashara 55 wa Tanzania wanaandamana na Mheshimiwa Rais Kikwete katika ziara yake ya siku tatu nchini Uturuki ambayo rasmi imemalizika . Mheshimiwa Rais Kikwete anatarajiwa kuondoka Uturuki , Jumapili, Februari 21, 2010, kwenda Jordan kwa ziara ya Kiserikali ya siku mbili.

Rais Kikwete ametoa majibu hayo baada ya kuwa ameulizwa nini hasa nia ya nchi kama China na Uturuki ambazo ghafla zimeonyesha hamu kubwa ya kushirikiana kwa karibu zaidi na kujenga mahusiano makubwa zaidi na Bara la Afrika ambalo kwa miaka mingi limekuwa karibu na nchi za Magharibi, na hasa zile ambazo zilizitawala nchi hizo za Afrika.

Rais Kikwete amesema kuwa hamu ya Bara la Afrika ni kuona maendeleo ya haraka kwa watu wake, na nchi yoyote duniani ambayo iko tayari kusaidia azma hiyo ya Afrika inakaribishwa kwa mikono miwili kufanya shughuli na Bara la Afrika.

“Tunaendesha mahusiano yetu kwa misingi ya ushirikiano (partnership) siyo kwa misingi ya nani alitutawala wakati gani. Hakuna nongwa katika hili,” amesema Rais Kikwete na kuongeza:

“Watawala wa nchi mbali mbali wamebadilika. Sera za nchi mbali mbali zimebadilika. Lakini mahitaji na maslahi ya Afrika yamebakia pale pale. Mahitaji yetu ni masoko kwa bidhaa zetu, uwekezaji katika chumi zetu, upatikanaji wa teknolojia kwa ajili ya maendeleo yetu na nafasi za kuendeleza uwezo wa Bara la Afrika kwa njia mbali mbali na hasa kupitia elimu.”

Rais Kikwete amesema kuwa Bara la Afrika linayo haki ya kutafuta majawabu ya mahitaji yake kutoka nchi yoyote katika pembe yoyote ya dunia na bila kuwekewa masharti kama zinavyofanya baadhi ya nchi.

Amewakumbusha waandishi hao kauli ya kiongozi wa zamani wa China, Hayati Deng Ziyao Ping, ambaye kuhusu maendeleo na nani wa kushirikiana naye katika kutafuta maendeleo, alipata kusema:

“Sijali paka anayo rangi gani ili mradi awe na uwezo wa kukamata panya.”

Rais Kikwete amesema kuwa wakati mwingine ni jambo la kushangaza kuwa baadhi ya nchi ambazo zimewekeza sana katika uchumi wa China na kuifanya nchi hiyo jambari la uchumi duniani, ndizo zinalalamikia nchi za Afrika kushirikiana na China.

Amesema kuwa ni jambo la ajabu kabisa kuwa nchi hizo hizo ambazo zinapiga kelele kuhusu ukaribu wa nchi za Afrika na China, ndizo hizo hizo ambazo zimeshirikiana kwa karibu sana na nchi hiyo ya China.

“Kama nchi hizi kweli zina wasiwasi kuhusu China kuwa na uhusiano wa karibu na Afrika, kwa nini hazina wasiwasi kwa nchi hiyo kuwa karibu na nchi hizo. Kwa nini iwe sawa kwa China kushirikiana na wakubwa hawa, lakini iwe siyo sawa kwa China kushirikiana na nchi za Afrika?”