Tuesday, March 25, 2014

Hacker Geohot Aajiriwa na Facebook

 
Geohot, hacker maarufu aliyejailbrake iPhone ameajiriwa rasmi na Mark Zuckerburg, yaani Facebook. Hacker huyu ambaye pia aliwahi kushitakiwa na Sony kwa shughuli za uchakachuaji baada ya kuihack PS3 na kuruhusu watumiaji kuweza kutumia DVD feki za kuchakachua. Facebook hawakuthubitisha Geohot atafanya kazi gani kwenye kampuni hiyo. Hacker huyu ambaye anatumia majina mbali mbali katika shughuli zake pevu ikiwa ni pamoja na million75, mil, dream na hax0r ameshafanya fujo nyingi sana katika ulimwengu wa kompyuta. Kijana huyu kwa sasa ana umri wa miaka 22 tu.
Jina alilopewa na wazazi wake ni George Francis Hotz. Katika kazi za karibuni kabisa alizofanya hacker huyu ni kujailbraik iPhone na iPod Touch kwa kutumia njia aliyoiita Blackra1n na pia kuifungua (sim unlock) simu hiyo kwa njia aliyooiita blacksn0w.
Alipoihack PS3 Sony walimpandisha kizimbani, hata hivyo mwezi wa nne mwaka huu Sony na Geohot walikubaliana nje ya mahakama na hivyo Sony kufuta kesi ile. Geohot alipewa sharti la kuto-hack tena PS3 ili kufutiwa kesi hiyo, sharti ambalo alilikubali. Ajira hii kwa dogo huyu ni hasara kubwa kwa wachakachuaji kwani watakosa mengi pale atakapotingwa na kazi za Facebook. Hacker huyu huwa hana noma, baada ya kufanya mambo yake huyaweka wazi kabisa katika tovuti yake ambayo ni www.geohot.com 
Kwa sasa kwenye tovuti yake ameacha ujumbe mfupi wa ajabu, waweza kwenda kuangalia mwenyewe.

No comments: