Tuesday, November 25, 2008

miriam odemba apongezwa jana usiku


Miriam Odemba akionesha Crown yake original kabisa aliovishwa mara baada ya kuibuka mshindi wa pili katika mashindano ya Miss Earth Air 2008 yaliyofanyika nchini Filpine hivi karibuni
Miriam akiwa na mama yake mzazi katika nyuso za furaha kabisa usiku huu kwenye hafla yake fupi ya kupongezwa kwa kuiletea hsehima kubwa Tanzania

Miriam akiwa amepozi na waheshimiwa usiku wa jana ndani ya hoteli ya New Africa,katika hafla ya kumpongeza mlimbwende huyo.kati ni baba yake mzazi Miriam Odemba pamoja na Prof Philimon Sarungi

Miriam akipongezwa na shangazi yake

"Hongera sana mwanangu kwa kutuletea heshima kubwa Tanzania"!

"Well done Miriam "



Miriam akiwa amepozi na wageni waalikwa mbalimbali ndani ya new africa hotel waliofika kumpongeza

Miriam Odemba akiwashukuru wageni waalikwa mbalimbali wakiwemo baadhi ya viongozi wa serikali waliofika kwenye hafla yake ya kumpongeza kwa ushindi alioibuka nao

Mama yake mzazi Miriam Odemba akiwashukuru wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye hafla hiyo fupi ikiwemo kampuni ya Campass Communication ambayo ilishiriki kwa kiasi kikubwa kumuandaa mlimbwende huyo



Mkurugenzi wa Kampuni ya Campass Communication Maria Sarungi akizungumza mbele ya wageni waalikwa kwenye hafla fupi ya kumpongeza mlimbwende wa Dunia namba 2 Miriam Odemba baada ya kuibuka mshindi wa pili katika mashindano ya miss Earth yaliyofanyika hivi karibuni nchini Ufilipino. Hafla hii imefanyika jana usiku ndani ya hoteli ya New Africa.Maria Sarungi alisema kuwa Odemba bado ana kazi kubwa inamkabiri mbele yake kuhakikisha taji hilo linabaki kwa Tanzania, kama vile haitoshi ameongeza kuwa Odemba pia atashiriki kufanya kazi mbali mbali za kijamii hapa nyumbani na pia desemba 28 atarejea nchini Filpine kuungana na mshindi wa kwanza katika kufanya kazi za kijamii nchini humo.Pia atatembelea nchi mbalimbali ikiwepo Singapore na nyinginezo.Aidha Maria amebainisha kuwa Miriam amepata mkataba wa mwaka mmoja wa kufanya kazi nchini humo

No comments: