Tuesday, November 25, 2008

mambo yameiva.!

Pichani shoto ni waliokuwa mawaziri Daniel Yona pamoja na Basil Mramba walipokuwa mahakama ya kisutu leo mchana jijini Dar.

Mawaziri wawili wa zamani Basil Mramba na Daniel Yona wamepandishwa kizimbani leo mchana mahakama ya kisutu na kusomewa mashitaka yao yapatayo 17 ya matumizi mabaya ya fedha pamoja na madaraka waliokuwa nayo,aidha watuhumiwa hao walipaswa kutoa bilioni 3.9 kesh,wadhamini wawili wa kuaminika pamoja kutoa pasi zao kusafiria na pia wametakiwa kutotoka nje ya Dar ikiwa ni masharti ya kupata dhamana.Kutokana moja ya masharti hayo kuwa magumu watuhumiwa hao wameshindwa kupata dhamana na hivyo kupelekwa rumande mpaka desemba 2.

No comments: