Thursday, August 27, 2009

sherehe za jeshi la wananchi kutimiza miaka 45
Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange akitoa maelezo kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya mambo ya nje Ulinzi na Usalama Wilison Masilingi mara baada ya ufunguzi wa maadhimisho ya JWTZ kutimiza miaka 45. Mh. Masilingi alikuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa Maadhimisho hayo yanayoendelea katika kikosi cha 603 cha jeshi eneo la Airwing ,Ukonga jijini Dar es salaam.Wa kwanza Kulia ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein mwinyi ambaye aliambatana na Naibu wake Dkt. Emannuel Nchimbi (wa kwanza kushoto).
Baadhi ya wananchi wakijitokeza kuangalia maonesho ya wiki ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) kutimiza miaka 45 wakipata maelezo kuhusu silaha za kivita kutoka kwa wataalam wa Jeshi hilo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya mambo ya nje, Ulinzi na Usalama Mh. Wilson Masilingi akipata ufafanuzi kutoka kwa Luten Kanali Anselum Bahati kuhusu bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na JWTZ kikosi cha Nyumbu wakati wa maonyesho ya miaka 45 ya JWTZ.Kushoto ni Mkuu wa Majeshi Generali Davis Mwamunyange


Wananchi wakijitokeza katika mabanda ya huduma za tiba kwenye maonyesho ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania kutimiza miaka 45
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye maonyesho ya JWTZ kutimiza miaka 45 wakipata huduma za tiba na ushauri leo katika mabanda ya Maonyesho katika viwanja vya kikosi cha 603 cha Jeshi la wananchi Air wing,Ukonga jijini Dar es salaam.




Mkuu wa Majeshi Generali Davis Mwamunyange na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya mambo ya nje Ulinzi na Usalama Wilison Masilingi (kushoto kwa afande Mwamunyange) wakipata maelezo mara baada ya ufunguzi wa maonesho na maadhimisho ya JWTZ kutimiza miaka 45. Mh. Masilingi alikuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa Maadhimisho hayo yanayoendelea katika kikosi cha 603 cha jeshi eneo la Airwing ,Ukonga jijini Dar
Askari wa kikosi cha anga katika maonesho hayo
Wanafunzi wakiangalia baadhi ya silaha katika maonesho hayo
Askari wenye silaha za kutungua ndege katika maonesho
Wananchi wakiangalia vifaa vya kijeshi kwenye maonesho hayo





No comments: