Monday, August 3, 2009

heka heka za kabla ya kuwasili kwa mwenge wa uhuru

Vijana wakifurahia kuwasili kwa menge wa uhuru
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Jordan Lugimbana akipita kuwasalimia viongozi mbalimbali
Maelekezo ya awali yalikuwa yakitolewa kabla ya Mwenge wa Uhuru kuwasili uwanja hapo.
Walikuwepo vijana mbalimbali kutoka mataifa ya nje ambao pia walifika kuupokea Mwenge wa Uhuru.

Ilikuwa ni furaha tu wanjani hapo
Vijana wakifurahia kwa mapokezi ya mwenge wa uhuru
Watu mbalimbali wakicheza na kuimba huku wakisubiri kuwasili kwa menge wa uhuru uwanjani hapo.
Wajasiliamali pia hawakukosa viwanjani hapo
Vijana kutoka Wilaya ya Kinondoni wakiimba nyimbo mbalimbali kuhusiana na Mwenge wa Uhuru uliowasiri jana jioni Kata ya Kawe katika viwanja vya Tanganyika Peka,Kinondoni jijini Dar.Mapokezi ya Mwenge huo yalikwenda sambamba na uhamasishaji wa mbinu mbalimbali za kupambana na ugonjwa wa UKIMWI ikiwemo na kupima afya kwa hiyari.
Pichani ni bendera za mataifa wakilishi mbalimbali zikiwa zinapepea
Mbio za Mwenge wa uhuru zilikuwa kata ya Kawe jana jioni katika viwanja vya Tanganyika Pekaz,ambapo watu mbalimbali wakiwemo viongozi wa serikali walihudhuria mapokezi ya mwenge huo wa Uhuru uliokuwa umebeba kauli mbiu ya "pinga unyanyasasi wa jinsia,watoto na mauaji ya albino".Mwenge huo ulipokelewa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Jordan Lugimbana.

No comments: