Friday, March 7, 2008

Ijue nguvu ya kuponya ya vyakula

SAMAKI (FISH)

• Huyayusha damu, huifanya kuwa nyepesi

• Huilinda mishipa ya damu isiharibike

• Huzuia damu kuganda

• Hushusha shinikizo la damu

• Hupunguza hatari ya kupatwa na mshituko wa moyo na kiharusi

• Hutuoa ahueni kwa wenye ugonjwa wa kipandauso

• Husaidia kuzuia uvumbe mwilini

• Huendesha mfumo wa kinga ya mwili

• Huzuia saratani

• Hutoa ahueni kwa wenye pumu

• Hupambana na dalili za awali za ugonjwa wa figo

• Huongeza nishati ya ubongo

KITUNGUU SAUMU (GARLIC)

• Hupambana na maambukizi

• Ina kemikali zenye uwezo wa kudhibiti saratani

• Hufanya damu kuwa nyepesi

• Hupunguza shinikizo la damu na kolestro

• Huamsha mfumo wa kinga ya mwili

• Huzuia na kutoa ahueni kwa kikohozi kilaini.

• Huweza kutumika kama dawa ya kifua

TANGAWIZI (GINGER)

• Huzuia ugonjwa wa kutetemeka

• Hufanya damu kuwa nyepesi

ZABIBU (GRAPE)

• Ina uwezo wa kufanya virusi visifanyekazi

• Huzuia meno kuoza

• Ina mchanganyiko wenye uwezo wa kuzuia saratani

PILIPILI HOHO (GREEN CHILLIES)

• Dawa nzuri ya mapafu

• Hutumika kama dawa ya kifua

• Huzuia na kuponya kikohozi kikali

• Husaidia kuyeyusha mabonge ya damu

• Hutoa maumivu

• Huweza kumfanya mtu kuwa na furaha

ASALI (HONEY)

• Huua vijidudu (bacteria)

• Huondoa wadudu kwenye vidonda na malengelenge

• Huondoa dalili za maumivu

• Hutoa ahueni kwa wagonjwa wa pumu

• Hutuliza maumivu ya vidonda vya koo

• Hutuliza mishipa ya damu, humpatia mtu usingizi

• Hutoa ahueni kwa mtu anayeharisha

MAZIWA (MILK)

• Huzuia ugonjwa wa mifupa (osteoporosis)

• Hupambana na maambukizi, hasa kuharisha

• Hurekebisha kuchafuka kwa tumbo

• Huzuia vidonda vya tumbo

• Huzuia kuoza kwa meno

• Huzuia mtu kupatwa na kikohozi

• Huongeza nishati ya ubongo

• Hushusha shinikizo la damu

• Hushusha kiwango cha kolestro mwilini

• Hudhibiti baadhi ya saratani

UYOGA (MUSHROOM)

• Hufanya damu kuwa nyepesi

• Huzuia saratani

• Hushusha kiwango cha kolestro

• Huchangamsha mfumo wa kinga ya mwili

• Hudhoofisha virusi

SHAYIRI (OATS)

• Dawa bora ya moyo

• Hushusha kolestro mwilini

• Hurekebisha sukari kwenye damu

• Ina mchanganyiko wa virutubisho unaodhibiti saratani

• Hupambana na kuvimba kwa ngozi

• Ina uwezo sawa na dawa ya kumpatia mtu choo

KITUNGUU MAJI (ONION)

• Dawa kubwa ya magonjwa ya moyo

• Huimarisha kolestro nzuri (HDL)

• Huifanya damu kuwa nyepesi

• Hushusha kiwango cha kolestro mbaya

• Huzuia damu kuganda

• Hurekebisha kiwango cha sukari kwenye damu

• Huua vijidudu

• Huzuia saratani

Ijue nguvu ya kuponya ya vyakula

Hapo zamani za kale kabla wanasayansi hawajavumbua dawa za kisasa kwa ajili ya kutibu magonjwa mbalimbali yanayomkabili binadamu, mababu zetu walikuwa wakitumia mitishamba na vyakula kutibu magonjwa ya aina yote yaliyokuwa yakiwakabili. Kwa maelfu ya miaka, chakula kimehesabika kama tiba ya matatizo mengi ya kiafya, hilo halina ubishi hadi leo.

Lakini katika karne iliyopita, dawa nyingi za kisasa zimevumbuliwa na kuchukua nafasi ya vyakula, hasa kutokana na uwezo wake wa kutibu ugonjwa haraka. Lakini madhara yatokanayo na matumizi ya muda mrefu ya dawa hizo, yameanza pia kuwafanya watumiaji wake kukimbilia tiba mbadala za mitishamba na vyakula ambavyo havina madhara katika afya ya binadamu na hutibu kwa uhakika.

Katika makala ya leo tutaangalia baadhi ya vyakula na nguvu ilivyonavyo katika kuzuia na kutibu magonjwa mbalimbali kama ilivyothibitishwa na tafiti mpya za kisayansi juu ya suala hili na kuelezwa na mwandishi Tanushree Podder katika kitabu chake cha You Are What You Eat:

APPLE (Tufaha)

• Dawa nzuri ya ugonjwa wa moyo

• Hushusha kolestro

• Hushusha shinikizo la damu

• Huimarisha kiwango cha sukari katika damu

• Huongeza hamu ya kula

• Linakemikali yenye uwezo wa kuzuia saratani

• Juisi yake inaua virusi vinavyoambukiza magonjwa

BANANA (NDIZI MBIVU)

• Huzuia na kutibu vidonda vya tumbo

• Hushusha kolestrol katika damu

BEANS (MAHARAGE YA AINA ZOTE)

• Hupunguza aina mbaya ya mafuta mwilini

• Hudhibiti kemikali mbaya za saratani

• Hudhibiti kiwango cha sukari kwenye damu

• Hushusha shinikizo la damu

• Hurekebisha mwenendo wa utumbo mkubwa

• Huzuia na kutibu ukosefu wa choo

• Huzuia kutokwa damu kwenye haja kubwa (haemorrhoids) na matatizo mengine ya tumbo

CABBAGE (KABICHI)

• Hupunguza hatari ya kupata saratani, hasa ya utumbo

• Huzuia na kutibu vidonda vya tumbo (hasa juisi yake)

• Huchangamsha mfumo wa kinga ya mwili

• Huua bakteria na virusi mwilini

• Huharakisha ukuaji wa mwili

CARROT (KAROTI)

• Inaaminika kuzuia saratani, hasa zitokanazo na uvutaji sigara, ikiwemo saratani ya mapafu.

• Hushusha kolestro katika damu

• Huzuia ukosefu wa choo (Constipation)

COFFEE (KAHAWA)

• Kahawa si kinywaji cha mtu kupenda sana kutumia, lakini kinapotumiwa kwa kiasi kidogo na kwa tahadhari, kina faida zake:

• Huboresha utendaji kazi wa ubongo

• Hutoa ahueni kwa wagonjwa wa asma (asthma)

• Hutoa ahueni kwa wenye homa

• Huongeza nishati ya mwili

• Huzuia meno kuoza

• Ina kemikali ambayo huzuia saratani kwa wanyama

• Hutoa uchangamfu

CORN (NAFAKA- MAHINDI, MCHELE, N.K)

• Zina aina fulani ya kemikali ambazo huzuia saratani

• Hupunguza hatari ya kupatwa na aina fulani za saratani, magonjwa ya moyo na kuoza kwa meno

• Mafuta yake hushusha kolestro mbaya mwilini

IJUE UWEZO ZAIDI WA KITUNGUU SAUMU NA TANGAWIZI KATIKA AFYA YAKO!

Katika maisha ya sasa, ni vizuri sana kujua kila unachokula kina faida au madhara gani mwilini mwako, kwani unachokula leo, ndicho kitakachokufanya uugue au uwe mzima kesho, tiba au madhara ya chakula hujijenga mwilini kidogokidogo na matokeo yake huonekana baada ya muda mrefu.

Kitunguu saumu kimekuwa kikitumika kama dawa ya mitishamba, takribani miaka 5,000 iliyopita. Historia inaonesha kuwa wafungwa wa nchini China walikuwa wanatakiwa kula kitunguu saumu kibichi kila siku asubuhi ili kuimarisha afya zao.

Aidha inaelezwa zaidi kuwa nchini Misri, watumwa walikuwa wakilishwa vitunguu saumu na vitunguu maji ili wapate nguvu za kujenga ‘ma piramid’. Vile vile vitunguu vilikuwa vinatumika kama dawa ya kufukuza majini na mapepo wabaya.

Ukiacha ushahidi huo wa kiasili kuhusu uwezo na umuhimu wa kitunguu saumu kiafya, utafiti wa kisayansi umegundua pia kuwa kishina kimoja cha kitunguu saumu kina dawa sawa na uniti 100,000 za vidonge vya Pennicillin ambayo ni karibu ya robo dozi ya vidonge hivyo na havina madhara yoyote katika mwili wa binadamu.

Kitunguu saumu kinaaminika kuwa na uwezo wa kuzuia aina mbalimbali za saratani, kama vile saratani ya tumbo, ngozi, matiti, koo na utumbo mkubwa. Aidha kitunguu saumu kina uwezo wa kudhibiti seli zisizaliane vibaya na kuleta madhara mengine mwilini.

Aidha, kitunguu saumu kina uwezo wa kushusha shinikizo la juu la damu, ili kupata matokeo yake katika kuponya maradhi hayo, unahitaji kuwa unakula angalau kitunguu saumu kimoja mpaka vitatu kila siku kwa muda wa miezi mitatu. Lakini hata utakapokula kiasi chochote utakachoweza kwa wale msio na maradhi yoyote, bila shaka mtakuwa mnajijengea kinga katika miili yenu.

Aidha ulaji wa vitunguu saumu vibichi, husaidia kurekeshi kiwango cha sukari kwa wagonjwa wa kisukari na manufaa yanapatikana zaidi kwenye vitunguu vibichi kuliko vya kupika au kukaanga. Vilevile unaweza kuchanganya asali na vitunguu saumu na kula pamoja kama dawa ya kuondoa mafua.

TANGAWIZI

Hii nayo ni dawa ya mitishamba yenye nguvu na maarufu sana nchini China, India na Japan. Imekuwa ikitumika katika nchi hizo kwa karne kadhaa na kuenea hadi Mashariki ya Kati, Spain na West Indies. Kwa mujibu wa historia yake, kwa mara ya kwanza Tangawizi ilitengenezwa nchini Jamaika ili kusaidia tatizo la ukosefu wa choo, kichefuchefu, ugonjwa unaotokana na kutembea kwa muda mrefu na uchovu wa asubuhi.

Tangawizi inaaminika kuwa na uwezo wa kuzuia kuchafuka kwa tumbo, kubana kwa kifua na kuumwa kwa kichwa. Kwa mujibu wa kitabu cha You Are What You Eat, katika bara la Asia, Tangawizi hutumika kuogea ili kuponya tatizo la kuziba kwa pua kutokana na mtu kuwa na ‘aleji’. Tangawizi husagwa na unga wake kutumika kuandaa kinywaji au inaweza kutumika ikiwa bado mbichi kwa kuwekwa kwenye maji ya moto na kunywa.

3 comments:

Anonymous said...

hi every person,

I identified kadidi2.blogspot.com after previous months and I'm very excited much to commence participating. I are basically lurking for the last month but figured I would be joining and sign up.

I am from Spain so please forgave my speaking english[url=http://wawhatsnewtoday.info/forum].[/url][url=http://thehottesttopicsou.info/].[/url][url=http://loweirdcrazymemories.info/forum].[/url]

Anonymous said...

Wow, that's what I was seeking for, what a data! present here at this webpage, thanks admin of this website.

Feel free to surf to my webpage; Trevon Mark

Anonymous said...

Hey, I think your website might be having browser compatibility issues.
When I look at your website in Ie, it looks fine but when opening in Internet Explorer, it has some overlapping.
I just wanted to give you a quick heads up! Other then that, great blog!


My blog post: Mekhi Dario