Tuesday, February 23, 2010

bongo darisalaaaaam...
Bwana Kadidi2i,
Kuna jambo ambalo limenitokea nikaamua kulileta kwako ili uweze kulitoa kwenye blog yetu ya hii huenda itasaidia wadau wengine manake hata mimi huaga najifunza mambo mengi sana kutoka kwenye blog hii.

Siku ya jmosi nilienda mjini kidogo kufanya shopping ya bidhaa nilizunguka sana nikapata kiu ya maji bahati nzuri nilipokua napita mitaa ya kisutu nikakutana na muuza maji alikuwa amebeba kwenye box lake maji ya aina ya uhai ikabidi ninunue alikua amebeba yale ya shilling 300/=.Nikanywa harakaharaka kwa sababu nilikua na kiu kali.

Baada ya kumaliza sikukitupa hicho kichupa cha plastic maaana sikuona mahali pa kutupia kwa hiyo nikaamua niende nacho mpaka nipate mahali pa kutupia.Nikawa nimekishika mkononi mara wakati naichezea mkononi nikahisi mikwaruzo kuangalia kumbe kile kichupa kilikuwa kimetumika nilipoangalia kwa makini ndani ya chupa nikaona uchafu na juu ya mdomo wake nikaona uchafu mweupemweupe...
Nakuambia,Michuzi niliishiwa nguvu.Nikapata mstuko mkubwa nikaenda mpaka pale mtaa wa Samora nilipokua nimepaki gari nikawa nimeduwaa sijui lakufanya.Wale vijana wanaokaaga pale kuongoza magari kupaki na saa nyingine kuosha magari wakaniuliza vipi?Nikawaeleza mkasa wote wakacheka sana wakaniambia umekunywa maji ya bomba sasa kilichobaki nikuomba Mungu usipate typhod.
Sasa wakaanza kunielimisha. Wakanieleza namna hayo maji vijana wa mjini wanavyoyatengeneza.
Kuna njia kuu mbili. Moja ni kuwa wanaokota hayo sijui niite makopo au vichupa vya plastic sehemu mbalimbali jijini wanajaza maji ya bomba au maji yoyote watakayopata halafu wanaenda kiwandani wananunua mifuniko pamoja na seal zake kabisa wanakuja wanasokomeza hiyo mifuniko pamoja na seal kwenye hivyo vichupa sasa wewe ukija kununua hayo maji ukafungua huo ufuniko lazima ikate seal kwa hiyo unapata imani unakunywa.

Njia ya pili wanaokota hivyo vichupa pamoja na mifuniko wanafungua wanajaza maji halafu wanachukua super glue wanaizungushia katikati ya mfuniko na seal yake wewe ukija kununua ukafungua utaona unakata seal kumbe ni super glue unakata.

Hii kitu ni hatari sana manake vichupa vyenyewe wameokota na hata kuviosha havijaoshwa kwa hiyo hapo mtu unakua na risk ya kupata TB,Typhod na magonjwa ya matumbo Kipindupindu.

Kwa hiyo wadau kuweni waangalifu na maji ya barabarani hasa ,wale vijana wanaobeba maji mikononi ambao wako katika mitaa mingi ya jijini Dar-es Salaam.Mfano maeneo hayo ya kisutu,kwenye mataa ya pale faya,manzese,ubungo na sehemu nyingine nyingi hasa zile sehemu zenye vituo au kwenye mataa.

Wako katika mitaa mingi ya jijini Dar-es Salaam.Mfano maeneo hayo ya kisutu,kwenye mataa ya pale faya,manzese,ubungo na sehemu nyingine nyingi hasa zile sehemu zenye vituo au kwenye mataa.

No comments: