Thursday, June 18, 2009

VODACOM KUMPATA MILIONEA ATAKAYEJIZOLEA TSH 100 MILIONI LEO
Vodacom Tanzania leo itampata milionea wake atakayejizolea Tsh 100 Milioni pesa taslimu katika droo kubwa itayorushwa moja kwa moja (LIVE) na kituo cha TBC1 kuanzia saa 3 usiku.
Mnamo mwezi Machi mwaka jana wa 2008, Vodacom Tanzania ilizindua promosheni ambayo kupitia zawadi zake zilizokuwa zinawagusa watu wengi, iliweza kutimiza malengo ya wateja wake.
Promosheni hii ilijulikana kama TUZO DROO iliyodumu mpaka mwezi Machi mwaka huu. Zawadi nzuri za kila wiki kama vile washindi 100 kupata muda wa maongezi wenye thamani ya Tsh 50,000 kila Mmoja pamoja na washindi 7 kujinyakulia Tsh 1 Milioni kila Mmoja.
Vilevile kulikuwa na zawadi za kila mwezi ambapo mshindi 1 aliweza kujizolea kitita cha Tsh 40 Milioni kila mwezi. Na mnamo mwezi Aprili mwaka huu, Vodacom ilizindua promosheni nyingine ikiwa ni mwendelezo wa promosheni ya TUZO DROO.
Promosheni hii ilijulikana kama TUZO MILIONEA ikiwa na zawadi ya muda wa maongezi wa Tsh 100,000 kwa mshindi mmoja kila siku. Promosheni hii ilikwisha Jumapili tarehe 14 Juni saa 5.59 usiku.
Vilevile, Vodacom iliweza kutangaza rasmi zawadi kubwa kabisa ya Tsh 100 Milioni itakayokwenda kwa mshindi Mmoja kwenye droo itakayochezeshwa leo hii usiku. Usikose kuwa mbele ya luninga yako kuanzia saa 3 usiku kwenye kituo chako bora cha TBC1 au DSTV chaneli 143 na ushuhudie ni nani atakayeibuka mshindi wa Tsh 100 Milioni pesa taslimu!!

No comments: