Mbowe;- Siongozi Genge La Wasaka Vyeo
Mwenyekiti
 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA  Freemaan Mbowe amesema 
kamwe haongozi kundi au genge la wasaka vyeo na madaraka ndani ya chama 
chake bali anaongoza kundi la watu wanaopenda mabadiliko.Kiongozi huyo 
amesema binafsi hawezi kwa sasa kusema atagombea Urais au Ubunge kwa 
sababu huu si muda wake hata kidogo.
Mbowe
 amesema mwanachama yeyote makini wa Chadema kwa sasa ni muda wa 
kuwaunganisha wanachama na watanzania kwa ujumla na wala si muda wa 
kuwagawa kukimbilia madaraka. Kiongozi huyo amesema ndiyo maana 
makamanda wote wakiongozwa na Dr Slaa wamejichimbia vijijini kwa kazi 
moja tu ya kueneza vuguvugu la mabadiliko-M4C.
No comments:
Post a Comment