Tuesday, January 17, 2012

Ni safari ya Regia Mtema

Maafisa Usalama wa Bunge (Sargent at arms) wakiwa wamebeba Sanduku lililohifadhi mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum CHADEMA kutoka Kilombero mkoani Morogoro, Marehemu Regia Mtema aliyefariki mwishoni mwa wiki iliyopita kwa ajali. Mwili huu ulikuwa unatolewa katika Hospitali ya taifa Muhimbili mapema leo kwenda Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam ambapo kunashughuli ya kuuaga mwili wa Marehemu kitaifa na baade kusafirishwa hadi Ifakara kwa Maziko yatakayo fanyika kesho.

Maafisa Usalama wa Bunge (Sargent at arms) wakiweka jeneza lenye mwili wa marehemu Mh Regia Mtema MB kwenye gari tayari kuelekea karimjee kwa heshima za mwisho asubuhi hii.


No comments: